Coronavirus: Tanzania yathibitisha mgonjwa wa kwanza wa corona

UMMYHaki miliki ya pichaEGAN SALLA- BBC
Image captionWaziri wa afya Tanzania, Bi. Ummy Mwalimu
Tanzania imethibitisha kisa kimoja cha virusi vya corona.
Mnamo tarehe Machi,15, msafiri huyo aliiingia Tanzania majira ya saa kumi jioni.
Mgonjwa aliyetangazwa ni mwanamke wa miaka 46 raia wa Tanzania, ambaye aliwasili kutoka Ubelgiji kwa ndege ya shirika la Rwanda.
Msafiri huyo aliondoka nchini tarehe 3,Machi 2020 ambapo kati ya tarehe 5-13 Machi alitembelea nchi za Sweden na Denmark na kurudi tena Ubelgiji.
Msafiri huyo alipita uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
Waziri Ummy Mwalimu amesema msafiri huyo alipofika KIA alifanyiwa ukaguzi na maafisa wa afya na kuonekana kutokuwa na homa.
Baadae alianza kujisikia vibaya akiwa hotelini na kwenda hospitali ya mkoa ya rufaa ya Mount Meru Arusha ambapo sampuli ilichukuliwa na kupelekwa maabara ya taifa ya afya ya jamii iliyoko Dar es salaam kwa ajili ya uchunguzi.
"Vipimo vya maabara vimethibitisha kuwa mtu huyo ana maambukizi ya ugonjwa wa corona, covid -19, Mgonjwa anaendelea vizuri na matibabu."
Waziri Ummy ameongeza kusema," Serikali inaendelea kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha kwamba ugonjwa huu unathibitiwa ili usisambae nchini.
Coronavirus: Je simu yako ni safi na salama
Aidha serikali inashirikiana na shirika la afya duniani-WHO na wadau katika kuendelea kutekeleza mikakati ya kukabiliana na ugonjwa huu".
Raia wametakiwa kuchukua tahadhari ya kujikinga na ugonjwa huu kadri wanavyopokea taarifa na elimu za mara kwa mara kwa njia mbalimbali.
Unaweza kutazama
Coronavirus: Tanzania yathibitisha kuwa na kisa cha kwanza

Tamko la serikali ya Tanzania

Kwa kuzingatia kanuni ya 46 ya sheria ya afya ya jamii ninaelekeza mambo yafuatayo:
  • Kwanza watanzania wasiokuwa na safari za lazima wanashauriwa kwa sasa kusitisha safari zao kwenye nchi zenye maambukizi
  • Taasisi zote zikiwemo shule, hoteli, maduka ya biashara, nyumba za kulala wageni, makanisa, misikiti, ofisi za umma na binafsi, vituo vya kutolea huduma za afya, taasisi za fedha, vyombo vya usafiri pamoja na maeneo ya mikusanyiko ya watu kama vile masoko, viwanja vya michezo na vituo vya abiria kuweka vifaa vya kunawia mikono kwa maji yanayotiririka na sabuni au maji yenye dawa kwa ajili ya kuhakikisha usafi wa mikono.
  • Kuweka maji yenye dawa ya chroline katika mageti ya kuingia katika hifadhi zote kwa ajili ya kusafisha mikono ya watalii na waongoza wageni.
  • Kuepuka kusalimiana kwa kushikana mikono
  • Kukumbatiana , kubusu, kuepuka kushika pua, mdomo na macho.
  • Hospitali zote nchini za serikali na zisizo za serikali kuweka zuio la idadi ya watu ambao wanakwenda kuwaona ndugu zao. Kwa maelekezo ya waziri ni kwamba wageni wa kumuona mgonjwa wasizidi wawili kwa siku kwa kila mgonjwa mmoja.
  • Wananchi wametakiwa kutoa taarifa kwa vituo vya afya iwapo watamuona na mtu mwenye dalili za ugonjwa wa Covid- 19.
Presentational grey line
Presentational grey line

Maoni ya watanzania katika mitandao ya kijamii

Hali hii imezua taharuki nchini humo kwa baadhi ya wananchi, huku wengine wakijilinganisha na hali hii wanavyoiona katika mataifa ya ulaya kama Italia.
Msaanii wa vichekesho wa Tanzania, Idris Sultan ameandika kwenye kurasa yake ya twitter na kuzua mjadala, watu wakiambiwa wakae nyumbani bila ya kufanya kazi wataweza kujikimu?
Katika hatua nyingine, serikali ya Somalia imetangaza kuwa na kisa cha kwanza cha virusi vya corona.

Ramani ya Coronavirus: Kasi ya kusambaa kwa virusi 17 Machi 2020

Maelezo haya yanatokana na data za mara kwa mara kutoka Chuo kikuu cha Johns Hopkins na huenda yasiangazie hali halisi ya mambo yalivyo katika kila nchi.
Jumla ya visa vilivyothibitishwaJumla ya vifo
181,9687,153
VisaVifo
Uchina81,0493,230
Italia27,9802,158
Iran14,991853
Uhispania9,942342
Korea Kusini8,32082
Ujerumani7,27217
France6,637148
Marekani4,59485
Uswizi2,33019
Uingereza1,54455
Netherlands1,41324
Norway1,3473
Sweden1,1217
Belgium1,0585
Austria1,0183
Denmark9143
Japan82527
Mili ya Diamond Princess6967
Malaysia566
Qatar439
Canada4134
Australia3773
Ureno3311
Ugiriki3314
Jamuhuri ya Czech298
Finland277
Israel255
Slovenia2531
Singapore243
Bahrain2141
Estonia205
Brazil200
Kashmir inayotawaliwa na Pakistan183
Iceland180
Poland1774
Ireland1692
Romania168
Chile155
Misri1502
Thailand1471
Ufilipino14212
Indonesia1345
Saudi Arabia133
Iraq12410
Kuwait123
India1192
San Marino1097
Lebanon993
Milki za Kiarabu98
Urusi93
Peru86
Luxembourg771
Slovakia72
Taipei ya China671
Afrika Kusini62
Vietnam61
Serbia57
Croatia57
Argentina562
Panama551
Brunei Darussalam54
Colombia54
Algeria544
Mexico53
Armenia52
Bulgeria522
lbania511
Uturuki47
Maeneo ya Wapalestina43
Hungary391
Ecuador372
Morocco371
Belarus36
Costa Rica35
Latvia34
Cyprus33
Georgia33
Malta30
Moldova29
Uruguay29
Sri Lanka28
Bosnia na Herzegovina25
Senegal24
Oman22
Afghanistan21
Tunisia20
Macedonia Kaskazini18
Visiwa vya Faroe18
Jordan17
Lithuania17
Venezuela17
Guiana ya Ufaransa16
Martinique151
Burkina Faso15
Azerbaijan151
Maldivers13
Jamuhuri ya Dominica11
Bolivia11
Jamaica10
Kazakhstan10
Kisiwa cha Reunion9
New Zealand8
Jersey8
Uzbekistan8
Bangaldesha8
Paraguay8
Rwanda7
Monaco7
Cambodia7
Ukrain71
Ghana6
Guadeloupe6
Honduras6
Ethiopia5
Cuba4
Guyana41
Liechtenstein4
Mongolia4
Trinidad and Tobago4
Cameroon4
Guam3
Puerto Rico3
Polynesia ya Ufaransa3
Saint Barthélemy3
Ushelisheli3
Kenya3
Aruba2
Guatemala21
Kosovo2
Namibia2
Nigeria2
Saint Lucia2
Saint Martin (Eneo la Ufaransa)2
Andorra2
Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo2
Benin1
Bhutan1
Visiwa vya Cayman11
Jamuhuri ya Afrika ya Kati1
Congo1
Cote d'voire1
Netherlands Antilles1
Equitorial Guinea1
Eswatini1
Antigua na Barbuda1
Greenland1
Guernsey1
Guinea1
Vatican1
Liberia1
Mauritania1
Mayotte1
Nepal1
Congo1
St St Vincent na Gradines1
Somalia1
Sudan11
Suriname1
Tanzania1
Bahamas1
Togo1
Gabon1

Post a Comment

0 Comments